Poems

Mgomba

Mgomba umelala chini: hauna faida tena,
Baada ya kukatwa na wafanya kazi
Wa bustani kwa kusita.
Watoto, kwa wasiwasi wanasubiri wakati wao
Bustanini hakuna kitu
Isipokuwa upepo fulani wenye huzuni,
Unaotikisa majani na kutoa sauti ya kilio. 
 
Hivyo ndivyo ufalme wa mitara ulivyo.
Mti wa mji umelala chini: hauna faida tena,
Baada ya kukatwa na wafanya kazi
Wa bustani kwa kusita.
Chumbani hakuna kitu
Isipokuwa upepo fulani wenye huzuni utingishao
Wenye hila waliokizunguka kitanda na kulia.
Machozi yenye matumaini yapiga
Mbiu ya hatari ya magomvi nyumbani.
           Magomvi
Kati ya wanawake
           Magomvi
Kati ya watoto kwa ajili ya vitu na uongozi.
Ole! Milki ya 'Lexanda imekwisha!
 
Vidonda vya ukoma visofunikwa
Ambavyo kwa mda mrefu vilifichama
Sasa viko nje kufyonzwa na inzi wa kila aina
Na vinanuka vibaya.
Lakini inzi kila mara hufyonza wakifikiri
Nani watamwambukiza.