Poems

Sauti?

Shingo zetu zimechongoka
            asubuhi kuilekea
lakini usiku wasogea
            ukichimba misingi ya nyumba,
                      na ukuta wa dakika nyumba
                      kuizunguka.
 
Kifo kimeadhimishwa
na ule wakati uliotandazika
                      mpaka
kila cha zamani kimesahaulika
isipokuwa majani makavu yalokauka
Mitini, mara kwa mara, yakitingisika
 
   Ati n'nani aliyesikia sauti?
   Kama kwamba kuna mtu huko mbinguni
wa kutulipia damu yetu iliyomwagwa
            na kumwagika