Poems

Mimi Ni Mimi

Waniita mkomunisti
Waniita mkapitalisti
Waniita mnashinalisti
Na mimi ni binadamu tu,
Kwani hilo halitoshi?
 
Nchi zinajiwakia
Mamama wakiomboleza, wakilia
Tumbi ya watoto wakiumia
na maneno yote tunayotumia
            kuuana na kuangamia
 
Ewe mto
Tumesimama pambizoni mwako
machozi yakitudondoka
            yakichanganyika moyoni mwako.